Our Blog

02 May

2022

Tuzo Za Shindano La Uandishi Wa Hadithi Fupi

Lengo kuu la maktaba hii ya Mwanawetu Books ni kuenzi na kuiendeleza lugha ya Kiswahili, katika kutimiza lengo hili, MBC imeshirikisha Wanafunzi wa ngazi ya Shule za Sekondari kufanyia kazi mada walizosoma wakiwa shuleni kuhusu Fasihi Simulizi na Fasihi Andishi.

Mada: Inatokana na kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani 2022 “SERIKALI YETU MADINI YETU” ambayo imetumika na taasisi zilizopo katika Kanda ya Ziwa.


Kwa nini kauli mbiu “Serikali yetu, madini yetu” itumike Kanda ya Kusini?

Maeneo mengi ya Kanda ya Kusini yanaonekana kuwa na migodi mingi ya madini mbalimbali, migodi hiyo imeweza kunufaisha jamii nyingi za Kitanzania na nje ya nchi. Mfano wa migodi hiyo ni mgodi wa shaba ya bluu Tunduru mkoani Ruvuma, makaa ya mawe wilayani Mbinga, Nyasa. Pia mkoani Lindi kuna migodi ya mawe ya gypsum wilayani Kilwa, gesi asilia Songosongo wilayani Kilwa na mgodi wa dhahabu na green tomalin wilayani Ruangwa, wakati mkoa wa Mtwara ukiongozwa na uchimbaji mkubwa wa gesi asilia na uzalishaji wa chumvi na chokaa.


1.1 Tunzo

Mshindi wa kwanza amepata zawadi ya fedha taslimu Tsh. 100,000/= pamoja na vifaa vya shule wakati washindi wengine 10 wamepata zawadi mbalimbali pamoja na fedha taslimu.

Hadithi 10 bora zitachapishwa kwenye maktaba yetu ya kidigitali inayopatikana mtandaoni kupitia; https://www.mwanawetubooks.co.tz

Washindi wote walitangazwa tarehe 08 Machi, 2022, katika sherehe ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.


1.2 Siri ya ushindi

1. Uwezo wa kuhusianisha hadithi, wahusika, na kaulimbiu ya Siku ya Wanawake Duniani “Serikali yetu madini yetu”
2. Matumizi ya visawe visivyotumika mara kwa mara na Wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili nchini Tanzania
3. Mtiririko na mpangilio wa visa na wahusika
4. Uwezo wa kuhusianisha kaulimbiu na maisha halisi ya wanawake waishio katika ukanda wa madini

Recent Posts

Wa Maajabu

Safari Ya Mikumi

Kiburi Chaponza

98 comments

  • Frank Mgimba

    NOVEMBER 06, 2021

    Very interesting story, thanks to the author of "Usimuache Atoke"

    Reply
  • Frank Mgimba

    NOVEMBER 06, 2021

    We need more of these stories for learning in a day to day life

    Reply
    • Mwanawetu-(Admin)

      NOVEMBER 06, 2021

      More book stories to come and we are working on bringing more to our audience for further learning and self development

      Reply
    • Mwanawetu-(Admin)

      NOVEMBER 06, 2021

      Keep on visiting our website for latest updates

      Reply
  • Frank Mgimba

    NOVEMBER 06, 2021

    Thank you

    Reply

Write Your Review

stay up-to-dated

Copyrights © 2022-mwanawetubooks.co.tz - All Rights Reserved